Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Raia wa Tanzania, DRC wapigwa marufuku kuingia Uingereza
Habari MchanganyikoTangulizi

Raia wa Tanzania, DRC wapigwa marufuku kuingia Uingereza

Spread the love

UINGEREZA imepiga marufuku abiria kutoka Tanzania na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kuingia nchini humo, ili kuzuia maambukizo ya aina mpya ya virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu …. (endelea).

Katazo hilo linaanza kwa wasafiri wote waliotoka ama kupita nchini Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ndani ya siku 10 zilizopita.

Waziri wa uchukuzi wa Uingereza, Grant Shapps, jana Alhamisi tarehe 21 Januari 2021, ameeleza katika ukurasa wake wa Twitter, “ili kusaidia kuzuia kuenea kwa aina ya COVID-19 iliyogundulika Afrika Kusini, tunapiga marufuku abiria wote wanaoingia kutoka Tanzania na DRC kuanzia saa 10 alfajiri kesho (Ijumaa).”

Hata hivyo, Shapps amesema, raia wa Uingereza na Ireland na wale kutoka mataifa mengine ambao wenye wanabali vya ukaazi, wataruhusiwa kuingia nchini humo, ila kwa sharti la kujitenga nyumbani pamoja na familia zao kwa muda wa siku 10 baada ya kuwasili.

(To help to stop the spread of the COVID-19 variant identified in South Africa, we are banning all arrivals from Tanzania and Democratic Republic of Congo from 4am tomorrow.

Tanzana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, zimeongezwa kwenye orodha ya Uingereza ya nchi zilizopigiwa marufuku ya wasafiri wake kuingia nchini humo kama hatua za kudhibiti maambukizo ya aina mpya ya virusi vya Corona vilivyogunduliwa nchini Afrika kusini.

Awali, mwezi huu mataifa mengine 11 ya Afrika yalipigwa marufuku kama hiyo. Mataifa hayo, ni Namibia, Zimbabwe, Botswana, Eswatini, Zambia, Malawi, Lesotho, Msumbiji na Angola, Shelisheli na Mauritius.

Abiria kutoka Afrika Kusini, walipigwa marufuku kuingia Uingereza, tarehe 24 Desemba mwaka jana.

Taifa la Uingereza ni miongoni mwa mataifa ambayo yanakabiliana na janga la virusi vya corona kwa kiwango kikubwa na uchumi wake ukiwa umeyumba kutokana na wimbi la kwanza la virusi mambukizi.

Wakati Uingereza ikitangaza kupiga marufuku raia wa Tanzania na DRC kuingia nchini humo, Ujerumani na baadhi ya nchi nyingine za Ulaya, walikuwa wakijadiliana uwezekano wa kufunga mipaka yao.

Serikali ya Tanzania imeondoa sharti wageni wanaoingia nchini humo kukaa karantini kwa muda wa siku 14, hata hivyo wanaowasili wote wanapimwa joto na endapo wataonesha dalili za COVID-19 ndio watahitajika kujitenga kwa muda wa siku 14.

Akitoa ujumbe wa shukurani kwa viongozi wa dini, Rais John Magufuli, aliwataka Watanzania wote kwa kuitikia wito wa kumuomba Mungu ili aliepushe taifa na janga la ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!