Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Raia wa Armenia kortini kwa kuisababishia Serikali hasara Mil. 44
Habari Mchanganyiko

Raia wa Armenia kortini kwa kuisababishia Serikali hasara Mil. 44

Spread the love

VARDAN MKHITARYAN (47), raia wa Armenia na mwenzake, wamefikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam kwa kosa kuisababishia hasara Serikali kiasi cha Sh. 44 milioni. Anaripoti Faki Sosi ,Dar es Salaam…(endelea).

Mwenzake ni Rosemary Mwemezi (32), Mtanzania .

Leo Jumatatu tarehe 8 Juni 2020, watuhumiwa hao wamesomewa mashtaka sita na Jacqline Nyantoli mbele ya Hakimu Mkazi Augustina Mbando.

Shtaka la kwanza ni la kula njama, linadaiwa kutendwa na washtakiwa wote wawili kati ya tarehe 1 Oktoba 2019 na tarehe 28 Mei 2020 kwenye maeneo tofauti jijini Dar es Salaam, kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la udanganyifu kupitia vifaa vya mawasiliano ya kieletroniki.

Kosa la pili, limetendwa na mtuhumiwa wa kwanza la kuingiza vifaa vya mawasiliano ya kieletroniki bila kuwa na kibali cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kosa hilo linadaiwa kutendwa tarehe 1 na 30 Oktoba 2019 jijini Dar es Salaam.

Kosa la tatu ni kusimika vifaa vya mawaliano ya kieletroniki bila kibali cha TCRA .

Inadaiwa mshtakiwa Mkhitaryan kutenda kosa hilo kati ya tarehe 1 na 30 Oktoba 2019 maeneo ya Mbezi Beach Dar es Salaam.

Kosa la nne ni kuendesha vifaa vya kieletroniki bila kibali cha mamlaka linamkabili mshitakiwa Mkhitaryan ambaye ni Meneja wa Kampuni ya Classic Mall iliyopo Mbezi Beach Dar es Salaam, anadaiwa kati ya tarehe 10 Oktoba 2019 na Tarehe 28 Mei 2020 aliendesha vifaa hivyo kwa ajili ya kupokea na kuhamisha mawasiliano  ya kimataifa .

Shtaka la tano, ni la kufanya udanganyifu kwa lengo la kukwepa gharama za kupokea na  kuhamisha mawasiliano ya kimataifa .

Shtaka hilo linawakabili watuhumiwa wote na kutendwa tarehe 10 Oktoba 2019, na tarehe 28 Mei 2020 eneo la Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Shtaka la sita  la kutumia vifaa vya  mawasiliano ya kieletrokini bila kuruhusiwa na TCRA linamkabili Mkhitaryan.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kutenda kosa tarehe 10 Oktoba 2019 na tarehe 28 Mei 2020 eneo la Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Shitaka la mwisho  ni kuisababishia Serikali na mamlaka hasara ya kiasi cha Sh. 44, 552, 175.

Kosa hilo linamkabili Mkhitaryan  na anadaiwa kulitenda tarehe 10 Oktoba 2019, na tarehe 28 Mei 2020 eneo la Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri hilo.

Hakimu Mbando ameahirisha kesi hiyo mpaka 10, Juni 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!