Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Pyramids waipiga mkwara Namungo FC
Michezo

Pyramids waipiga mkwara Namungo FC

Kocha wa Pyramids FC, Rodolfo Arrubarrena
Spread the love

 

KUELEKEA mchezo wao dhidi ya Namungo FC, kocha wa kikosi cha Pyramids FC, Rodolfo Arrubarrena pamoja na nahodha wake, Abdallah El Said wamejitanabaisha kuwa wamekuja Tanzania kuchukua pointi tatu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo huo wa Kombe la Shirikisho Afrika wa Kundi D, utachezwa kesho tarehe 17 Machi, 2021 majira ya saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akiongea kwenye mkutano wa waandishi wa habari hii leo, jijini Dar es Salaam kocha wa Pyramids, Arrubarrena, alisema kuwa wamejikita kwenye mchezo huo kwa ajili ya kuchukua pointi tatu.

“Tumejiandaa kwa mchezo huo na lengo ni kuchukua pointi tatu na wachezaji wapo tayari kwa ajili ya mchezo,” alisema kocha huyo.

Kwa upande wa nahodha, Abdallah El Said, amesema kuwa wamekuja hapa kuchukua pointi tatu licha ya kujua kwamba timu nyingi za Tanzania zinacheza mpira mzuri na haitakuwa mechi rahisi.

“Tumekuja hapa kuchukua alama tatu na najua timu nyingi za Tanzania zinacheza mpira mzuri, najua haitakuwa mchezo rahisi na tutafanya kila lililowezekana kuondoka na alama tatu,” alisema Nahodha huyo.

Huu utakuwa mchezo muhimu kwa Namungo kwenye kundi hilo, kutokana na kupoteza katika mchezo wa kwanza dhidi ya Raja Casablanca uliofanyika nchini Morocco.

Namungo wanashika nafasi ya tatu kwenye kundi hilo huku akiwa hana pointi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!