PRESHA imeshuka. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya wanafunzi 682 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliofutiwa usajili kutakiwa kurejeshwa. Anaandika Regina Mkonde … (endelea).
Kauli ya kurejeshwa kwa wanafunzi hao imetolewa leo tarehe 22 Oktoba 2018 na Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Prof. Ndalichako ametoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo ya wahasibu yanayoendelea Dar es Salaam na kwamba, kauli ya kusimamishwa usajili wa wanafunzi hao aliisikia mwishoni mwa wiki iliyopita.
Prof. Ndalichako tayari ametoa maagizo kwa uongozi wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) na uongozi wa UDSM kukaa na kuangalia namna ya kumaliza suala hilo bila kuathiri wanafunzi hao.
Amefafanua kwamba, UDSM kuna nafasi 3,000 na kwamba, kilichotokea ni tatizo la kiufundi kutokana na wanafunzi wengi kupenda chuo hicho.
“Wanafunzi wengi wanapenda kusoma UDSM na tatizo lilikuwa linaweza kurekebishika na wote ni idara za serikali,” amesema Prof. Ndalichako na kuongeza;
“TCU na UDSM hawakutakiwa kushindana na ndiyo maana nimewaagiza hadi Jumamosi wawe wamemaliza tofauti zao.”
Leave a comment