Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Ndalichako anusa harufu ya ufisadi Kagarwe
Elimu

Prof. Ndalichako anusa harufu ya ufisadi Kagarwe

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akikagua chuo cha Ufundi Karagwe

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, amemwagiza Mwenyekiti wa Bodi ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, Peter Maduki kuunda tume ya kuhakiki matumizi ya Sh.4.65 bilioni katika ukarabati na ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi Karagwe Mkoa wa Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kagera … (endelea).

Profesa Ndalichako ametoa maagizo hayo hivi karibuni baada ya kukagua ukarabati na ujenzi  unaoendelea  wa chuo hicho ambao umepangwa kutumia kiasi hicho cha fedha mpaka utakapokamilika.

Chuo hicho kimekabidhiwa kwa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ili iweze kukisimamia na kukiendesha.

Ametaka uhakiki huo ufanyike ndani ya kipindi cha wiki mbili (siku 14) ili kuokoa fedha hizo ambapo mpaka sasa Mkandarasi ambaye ni Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ameshalipwa Sh.2.228 bilioni sawa na asilimia 48 ya gharama ya mradi huku mshauri elekezi EZM Architects and Associates akiwa amelipwa Sh.130.89 milioni.

Profesa Ndalichako amesema, baada ya kutembelea majengo haya na kuangalia gharama “sijaridhishwa kabisa, nikiangalia majengo haya, sijaridhika kabisa. Hatujawatendea haki watu wa Karagwe. Ikizingatia majengo yamejengwa kwa tofali za kuchoma ambalo moja ni Sh.80, kweli Sh.4 bilioni hapa, tumwogope Mungu.”

“Hapa sioni thamani ya fedha zilizokuja na majengo, ninakuagiza mwenyekiti na bahati nzuri fedha nyingi haijalipwa, fanya uhakiki ndani ya wiki mbili na bahati nzuri anayejenga ni TBA ambaye ni serikali. Ukaguzi ufanyike,” amesema Profesa Kabudi.

Waziri huyo amesema, Serikali imejenga na kukamilisha jumla ya Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi Stadi 41 huku vingine 29 vikiendelea kujengwa nchini, lengo ni kufanikisha mkakati wa kujenga uchumi wa viwanda na kufikia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025.

Amewataka wananchi kutambua umuhimu wa mafunzo ya ufundi stadi na kuwahamasisha vijana kujiunga na mafunzo hayo ili waweze kujipatia ajira kwa urahisi na kujikwamua kiuchumi lakini pia kuchangia juhudi za serikali kwa kuchangia pato la Taifa  kwa kulipa kodi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!