Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Mwakalila awafunda wanafunzi Chuo Mwalimu Nyerere, “ulipaji ada ni muhimu”
Elimu

Prof. Mwakalila awafunda wanafunzi Chuo Mwalimu Nyerere, “ulipaji ada ni muhimu”

Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Profesa Shadrack Mwakalila akizungumza na wanafunzi wa mwaka wa kwanza chuoni hapo pichani hapo.
Spread the love

 

MKUU wa Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere (MNMA), Profesa Shadrack  Mwakalila amewataka wanafunzi wa mwaka wa kwanza wa masomo kwa mwaka 2022/20223 kuzingatia zaidi masomo ikiwa ni pamoja na kusoma kwa bidii, juhudi na maarifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Aidha, Profesa Mwakalila amewataka wanafunzi hao kuwa waadilifu, waaminifu na kuzingatia suala la ulipaji  ada kwa wakati.

“Suala la kulipa ada ni la muhimu sana, kabla ya kuja hapa chuoni kila mmoja alijipanga kuja kusoma, hili siyo jambo la dharura na ilikuwa ni mipango ya muda mrefu hivyo ni wajibu ada ilipwe kwa wakati,” alisistiza Profesa Mwakalila.

Mkuu huyo wa Chuo amewataka pia wanafunzi hao kujiepusha na udanganyifu wa aina yoyote pindi wanapokuwa  chuoni.

Pia amewataka kujiepusha na mambo ambayo hayawezi kumsaidia  katika masomo, na migogoro yoyote au makundi ya uchochezi na suala zima la kuheshimiana kati ya walimu  na wanafunzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!