Saturday , 3 June 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Muhongo apinga TAMISEMI kusimamia elimu
Elimu

Prof. Muhongo apinga TAMISEMI kusimamia elimu

Prof. Sospeter Muhongo, Mbunge wa Musoma Vijijini
Spread the love

 

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ameshauri masuala ya elimu kusimamiwa na wizara moja badala ya wizara mbili, akisema suala hilo linachangia maendeleo yake kudorora. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Prof. Muhongo ametoa ushauri huo Jana Alhamisi, bungeni jijini Dodoma, akichangia Bajeti pendekezwa ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa 2023/24.

Prof. Muhongo amesema masuala ya elimu ya msingi na sekondari inapaswa kusimamiwa na wizara moja, huku akishauri iundwe Wizara ya Elimu, Sayansi, Utafiti na Uvumbuzi.

Kwa sasa masuala ya elimu yanasimamiwa na Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

“Elimu yetu iko na hali mbaya na hakuna wa kumalumi, muda umefika na pendekezo langu ni kwamba elimu ya msingi na sekondari kuipeleka Wizara Ofisi ya Rais TAMISEMI matokeo yake siyo mazuri na tumerudi nyuma. Nashauri masuala ya elimu yarudishwe Wizara ya Elimu,” amesema Prof. Muhongo.

Pia, Mbunge huyo wa Musoma Vijijini, ameshauri miundombinu ya elimu hususan madarasa, maktaba na maabara viboreshwe ili wanafunzi wapate elimu bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Serikali yatoa Sh. 573 mil. kukamilisha wa ujenzi sekondari ulioanzishwa na wanakijiji

Spread the love  SERIKALI kupitia Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI, imetenga Sh....

Elimu

CBE yaja na kozi mpya 16 zikiwemo za ujasiriamali na uvumbuzi

Spread the loveChuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kuanzia mwaka wa masomo...

Elimu

SUA kuhakikisha tafiti zinazofanywa zisiachwe kwenye makabati

Spread the love  MRATIBU wa utafiti na machapisho katika kurugenzi ya uzamiri,...

Elimu

Watakaopata Division One St Anne Marie Academy kupewa iphone ya macho matatu

Spread the loveMkurugenzi wa shule za St Anne Marie Academy, Dk. Jasson...

error: Content is protected !!