Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Muhongo apinga TAMISEMI kusimamia elimu
Elimu

Prof. Muhongo apinga TAMISEMI kusimamia elimu

Prof. Sospeter Muhongo, Mbunge wa Musoma Vijijini
Spread the love

 

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ameshauri masuala ya elimu kusimamiwa na wizara moja badala ya wizara mbili, akisema suala hilo linachangia maendeleo yake kudorora. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Prof. Muhongo ametoa ushauri huo Jana Alhamisi, bungeni jijini Dodoma, akichangia Bajeti pendekezwa ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa 2023/24.

Prof. Muhongo amesema masuala ya elimu ya msingi na sekondari inapaswa kusimamiwa na wizara moja, huku akishauri iundwe Wizara ya Elimu, Sayansi, Utafiti na Uvumbuzi.

Kwa sasa masuala ya elimu yanasimamiwa na Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

“Elimu yetu iko na hali mbaya na hakuna wa kumalumi, muda umefika na pendekezo langu ni kwamba elimu ya msingi na sekondari kuipeleka Wizara Ofisi ya Rais TAMISEMI matokeo yake siyo mazuri na tumerudi nyuma. Nashauri masuala ya elimu yarudishwe Wizara ya Elimu,” amesema Prof. Muhongo.

Pia, Mbunge huyo wa Musoma Vijijini, ameshauri miundombinu ya elimu hususan madarasa, maktaba na maabara viboreshwe ili wanafunzi wapate elimu bora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!