Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Muhongo aibana Halmashauri ya Musoma
Habari za Siasa

Prof. Muhongo aibana Halmashauri ya Musoma

Prof. Sospeter Muhongo, Mbunge wa Musoma Vijijini
Spread the love

 

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, mkoani Mara, kutumia mapato yake ya ndani kukamilisha miradi ya maendeleo iliyokwama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Prof. Muhongo ametoa wito huo Leo tarehe 12 Mei 2023, mkoani Mara.

Miongoni mwa miradi iliyokwama ni pamoja na, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya inayojengwa kwenye Kitongoji cha Kwikonero, makao makuu ya halmashauri, pamoja na kurekebisha vituo vya Afya vilivyojengwa chini ya viwango.

“Halmashauri itekeleze ipasavyo miradi ya maendeleo ya wanakijiji kwa kutumia mapato ya ndani. Halmashauri yetu itambue michango ya wadau wa maendeleo ikiwemo ya mbunge na ya wanavijiji kwenye miradi ya maendeleo inayotekelezwa Vijijini,” amesema Prof. Muhongo.

Katika hatua nyingine, Prof. Muhongo ameitaka halmashauri hiyo ijiepushe kupata hati chafu, huku akitaka itoe maelezo ya kina kuhusu hati chafu zilizopatikana.

“Ripoti za matumizi mabaya ya fedha za umma zitolewe haraka,” amesema Prof. Muhongo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!