Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Prof. Muhongo agawa msaada kwa wananchi waliokumbwa na mafuriko
Tangulizi

Prof. Muhongo agawa msaada kwa wananchi waliokumbwa na mafuriko

Spread the love

 

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, ametoa msaada wa dharura ikiwemo vyakula, kwa wananchi walioathirika na mafuriko ya mvua jimboni humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mbunge Jimbo la Musoma Vijijini, Prof. Muhongo ametoa msaada huo katika Kijiji cha Kusenyi, Kata ya Suguti, jana tarehe 4 Aprili 2023.

“Mbunge ametembelea Kijiji cha Kusenyi kutoa pole kwa waathirika wa mafuriko ya juzi na jana. Kushuhudia uharibifu uliotokana na mafuriko hayo na kugawa chakula cha dharura. Ametoa gunia 25 ya mahindi na maharage kilo 100,” imesema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imetaja vitongoji vilivyoathirika ikiwemo Nyabweke ambapo kaya 26 zimekumbwa na maafa hayo na kitongoji cha Kwikutu ambacho kaya 24 zimeathirika.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tathmini ya uharibifu wa mafuriko hayo inaendelea kufanywa, ambapo matokeo ya awali yanaonyesha baadhi ya nyumba zimebomoka, baadhi ya kaya chakula chao kilichohifadhiwa kimesombwa.

Tathmini ya awali inaonyesha kuwa, chanzo cha mafuriko hayo ni ujenzi wa barabara ya lami yenye urefu wa kilomita tano, kutozingatia uwekaji wa njia za kutosha za kupitisha maji, pamoja na wakulima wa mpunga kuweka miundombinu inayozuia maji kutiririka kwenye mikondo inayoelekea ziwani.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Prof. Muhongo ametoa wito kwa wananchi na wadau wa maendeleo kuendelea kuwasaidia wahanga wa mafuriko hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!