Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Mkenda: Wanasiasa msitupelekeshe
Habari za Siasa

Prof. Mkenda: Wanasiasa msitupelekeshe

Charles Mwijage, Waziri wa Viwanda, Biashara
Spread the love

PROFESA Adrof Mkenda, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, amewataka wanasiasa hapa nchini kuacha kuingilia masuala ya kitaalam yanayofonywa kwa kuzingatia utashi wa kitaaluma zaidi, anaandika Dany Tibason.

Pia amewaasa watumishi wa serikali kutokuwa tayari kufuata matakwa ya wanasioasa na badala yake wazingatie maadili na misingi ya kitaaluma katika majukumu yao.

Prof. Mkenda ameyasema hayo leo wakati akifungua semina ya wakurugenzi wa mipango na sera kutoka wizara mbalimbali iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hazina mjini Dodoma.

“Katika kufanya kazi za kutengeneza mipango na sera mbalimbali za kulinda ubora wa mlaji pamoja na usambazaji wa bidhaa, ni lazima tujiepushe na matakwa ya wanasiasa ambayo yamekuwa yakiingilia kazi za wataalam,” amesema.

Prof. Mkenda amesema ili kuimarisha ubora wa bidhaa nchini lazima mamlaka husika zinatakiwa kufanya ukaguzi wa bidhaa huku wakitoa elimu kwa jamii badala ya kutumia mabavu na mashambulio kwa watu ambao wanatoa huduma mbalimbali.

Amesisitiza kuwa, katika nchi ya Tanzania kuna sheria ya kufanya biashara huria lakini hairuhusu kuwa na biashara holela ili kulinda afya za walaji.

“Ili uweze kufanya ukaguzi wa bidhaa kwa uaminifu ni lazima ujipambanue na kujiondoa katika viashiria vya rushwa. Kupenyeza rushwa kunaweza ni chanzo kikubwa cha kuzagaa kwa bidhaa bandia mitaani.

“Tujiulize wale askari walioruhusu gari lililosababisha vifo vya watoto 32 walimu 2 na dereva mmoja wa Shule ya msingi ya Lucky Vincent ya Arusha hawakuona kama watoto wamezidi katika gari hiyo na walikuwa wamevunja sharia? uzembe unaweza kuligharimu Taifa,” amesema Prof. Mkenda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!