Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Mkenda aagiza uchunguzi wa kina shule zilizofanya udanganyifu
Elimu

Prof. Mkenda aagiza uchunguzi wa kina shule zilizofanya udanganyifu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda
Spread the love

 

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amemuagiza Kamishna wa Elimu kufanya uchunguzi wa kina kwa shule nne zilizobainika kufanya udanganyifu mkubwa katika mtihani wa kidato cha nne mwaka 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Prof. Mkenda amesema hayo alipokutana na wazazi na walezi wa wanafunzi waliofutiwa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne 2022 wa Shule ya Sekondari Thaqaafa ya Jijini Mwanza kwa ajili ya kuwasikiliza.

Amezitaja shule hizo kuwa ni Cornelius ya Kinondoni Dar es Salaam, Thaqaafa ya Mwanza, Mnemonic ya Zanzibar na Twibhoki iliyoko Mara na kumtaka Kamishna huyo kuchukua hatua kali kulingana na ripoti ya uchunguzi huo.

Mkenda amesisitiza wazazi kuwalea watoto katika maadili ili watambue kuwa udanganyifu si mzuri na una madhara makubwa katika upande wa haki, maadili na weledi.

“Tunapowapeleka watoto shule tunataka wajifunze waelewe ili baadae waje watumikie taifa. Sasa mtu anakuja kuwa daktari au mhandisi au rubani kwa kuiba mtihani, madhara yake ni makubwa sana,” ameongeza Mkenda.

Mkenda amewapa pole wazazi na kuwataarifu kuwa mitihani hiyo imefutwa na hivyo kilichopo ni kurudia mitihani.

“Kuhusu kurudia mtihani tumewasikiliza maombi yenu, ninashukuru kuwa hamna anayesema ameonewa sote tunakubaliana kuwa kulikuwa na udanganyifu na hivyo niseme matokeo yamefutwa na kikubwa ni maombi ya kurudia mtihani. Hili tunalichukua tutawasiliana nanyi baada ya kulifanyia kazi kwani ni suala la kibajeti pia,” amefafanua Mkenda.

Naye Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, akiwa katika kikao hicho amesema Serikali haitalea shule zinazofanya udanganyifu wa mitihani na kuongeza kuwa wanafunzi wanatakiwa wapimwe kwa uwezo na sio kwa kudanganya.

Katika maelezo yao yaliyotolewa kupitia Mwenyekiti wa wazazi hao, Patrick Msagati wameomba Serikali kuwahurumia na kuruhusu matokeo kuachiliwa au kuwapa nafasi ya kurudia mtihani.

“Tunaomba Serikali ichukue hatua kali kwa shule kama hizi kwani zimetusababishia madhara makubwa sisi kama wazazi na watoto pia. Ikiwezekana shule hizi zifungiwe,” amesema Michael Zayumba, mmoja wa wazazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!