STEVEN Ngonyani aliyefahamika zaidi kwa jina la Profesa Majimarefu, Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), amefariki dunia leo usiku Jumatatu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Ofisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Aminiel Eligaeshi amethibitisha kutokea kwa kifo cha mbunge huyo aliyekuwa amelazwa hospitalini hapo.
Prof. Majimarefu alianza kuugua akiwa bungeni jijini Dodoma tangu mwezi uliopita kabla ya kuhamishiwa Muhimbili Juni 20, mwaka huu. Ugonjwa uliokuwa ukimsumbua mbunge huyo hakikuwekwa wazi.
Leave a comment