Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba: Nipo tayari kung’oka CUF
Habari za Siasa

Prof. Lipumba: Nipo tayari kung’oka CUF

Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), amefungua milango kwa mwanachama mwenye uwezo kujitokeza na kugombea nafasi aliyonayo sasa. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kiongozi huyo ameeleza leo tarehe 25 Septemba 2018 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaama na kwamba, wakati wa kutafuta viongozi wapya unajongea hivyo wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali ikiwa ni pamoja na uenyekiti wanapaswa kujiandaa.

Prof. Lipumba amesema kuwa, hang’ang’anii madaraka na kwamba, atakayejitokeza kuwania nafasi hiyo lazima awe na uwezo na akubalike kwa wanachama.

“Sing’ang’anii madaraka, nitaondoka lakini anayetaka nafasi hii lazima awe na uwezo pia akubalike kwa wanachama,” amesema Prof. Lipumba na kuongeza;

“CUF ni chama kinachofuata demokrasia kwa uwazi wake. Mpaka sasa hakuna mtu aliyejitokeza kutaka nafasi ya uenyekiti ambaye atapitishwa na kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.”

Hata hivyo, amegusia taarifa za Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Shariff Hamada kutaka kuhamia Chadema ambapo amesema, hata akihama, hatodhoofisha CUF Zanzibar kwa kuwa ndio ilipo mizizi ya chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!