MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba amefanya mabadiliko madogo ya wakurugenzi wa chama hicho. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Prof. Lipumba amefanya mabadiliko hayo leo Jumatatu, tarehe 23 Agosti 2021.
“Baada ya kushauriana na Makamu Mwenyekiti wa Tanzania Bara, Maftah Nachuma na Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Zanzibar, Mussa Haji Kombo, nimefanya mabadiliko madogo ya wakurugenzi,” imesema taarifa ya Prof. Lipumba.
Katika mabadiliko hayo, Prof. Lipumba amemteua Khamis Mohamed Faki, kuwa4 Naibu Mkurugenzi wa Habari.
Taarifa ya uteuzi huo imesema, Faki anachukua nafasi ya Mbarouk Seif Salim ambaye ni Kaimu Naibu Katibu Mkuu.
Pia, Prof. Lipumba ameteua Rajab Mbarouk Mohamed, kuwa Mkurugenzi na Katibu wa Kamati ya Itifaki na Udhibiti, akichukua nafasi ya Thinney Juma Mohammed, ambaye anabaki na jukumu la kuwa mshauri wake maalum.
“Uteuzi huu utafikishwa kwenye kikao kijacho cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kwa kuthibitishwa,” imesema taarifa ya Prof. Lipumba.
Taarifa ya Prof. Lipumba imesema, amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa katiba ya CUF, toleo la 2014 Ibara ya 91 (1) (f), inayompa mamlaka ya kufanya hivyo kwa kushauriana na makamu mwenyekiti.
Leave a comment