Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba alalamika rafu Uchaguzi Liwale
Habari za Siasa

Prof. Lipumba alalamika rafu Uchaguzi Liwale

Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, anadai kuna uwepo wa rafu katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Liwale unaotarajiwa kufanyika tarehe 14 Oktoba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 9 Oktoba 2018 jijini Dar es Salaam, Prof. Lipumba amedai kuwa, kuna njama zinazofanywa na baadhi ya watumishi wa umma kwa minajili ya kukibeba Chama cha Mapinduzi CCM katika kulitwaa jimbo la Liwale kupitia uchaguzi huo.

Prof. Lipumba ameeleza kuwa, CCM inatambua kwamba CUF ina nguvu Liwale na hivyo inataka kutumia nguvu kulichukua jimbo hilo lililowazi baada ya ya aliyekuwa mbunge wake, Zubeir Kuchauka kujiuzulu na kurudi CCM.

Kufuatia madai hayo, Prof. Lipumba ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufuatilia kwa ukaribu mwenendo wa uchaguzi huo ikiwemo maandalizi yake kwa ajili ya kuzuia njamana ili uwe wa haki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!