Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba alalamika rafu Uchaguzi Liwale
Habari za Siasa

Prof. Lipumba alalamika rafu Uchaguzi Liwale

Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, anadai kuna uwepo wa rafu katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Liwale unaotarajiwa kufanyika tarehe 14 Oktoba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 9 Oktoba 2018 jijini Dar es Salaam, Prof. Lipumba amedai kuwa, kuna njama zinazofanywa na baadhi ya watumishi wa umma kwa minajili ya kukibeba Chama cha Mapinduzi CCM katika kulitwaa jimbo la Liwale kupitia uchaguzi huo.

Prof. Lipumba ameeleza kuwa, CCM inatambua kwamba CUF ina nguvu Liwale na hivyo inataka kutumia nguvu kulichukua jimbo hilo lililowazi baada ya ya aliyekuwa mbunge wake, Zubeir Kuchauka kujiuzulu na kurudi CCM.

Kufuatia madai hayo, Prof. Lipumba ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufuatilia kwa ukaribu mwenendo wa uchaguzi huo ikiwemo maandalizi yake kwa ajili ya kuzuia njamana ili uwe wa haki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!