Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Prof. Lipumba ajitosa mauaji Palestina
Kimataifa

Prof. Lipumba ajitosa mauaji Palestina

Spread the love

 

MWENYEKITI wa Chama Cha Wananchi (CUF), nchini Tanzania, Prof. Ibrahim Lipumba, ameishauri Serikali ya Tanzania, ifuate nyayo za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, za kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya raia wa Palestina. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Prof. Lipumba ametoa wito huo leo Jumatano, tarehe 19 Mei 2021, siku nane baada ya kuibuka mapigano katika Ukanda wa Gaza, kati ya Jeshi la Israel na wanamgambo wa Palestina, yaliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 200.

“Tunatoa wito kwa Serikali ya Tanzania, kurejea kwenye msimamo wa Mwalimu Nyerere wa kupinga dhulma na uonevu duniani kote na kuwaunga mkono kwa dhati Wapalestina wapate haki zao,” amesema Prof. Lipumba.

Akizungumzia mzozo huo wa muda mrefu baina ya Palestina na Israel, Prof. Lipumba amekumbushia uamuzi wa Mwalimu Nyerere wa kuitenga Israel kufuatia sera zake zinazodaiwa kuwakandamiza raia wa Palestina.

“Tanzania chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, ina historia ndefu ya kutetea na kupigania haki za Wapalestina,” amesema Prof. Lipumba.

Mwanasiasa huyo amesema “baada ya vita vya Yom Kippur baina ya Waarabu na Israel ya Oktoba 1973, Tanzania ilivunja uhusiano na Israel na kuunga mkono Wapalestina na mataifa ya Kiarabu ambayo ardhi yao iliporwa na Israel.”

Kuhusu mauaji yanayoendelea Gaza, Prof. Lipumba amesema, chama chake kinalaani mauaji hayo

“CUF tumesikitishwa na kukasirishwa na mauaji ya kinyama yanayofanyiwa Wapalestina katika ukanda wa Gaza kwa kupiga mabomu makazi ya wananchi na kusababisha vifo vya Zaidi ya watu 200 wakiwemo zaidi ya watoto 60.”

Israel na Palestina ziko kwenye mgogoro wa muda mrefu, uliosababishwa na kugombania ardhi.

1 Comment

  • Hongera Profesa Lipumba kwa kujitokeza na kuzungumzia suala hili linaloepukwa na wanasiasa wa CCM na wa Upinzani. Umesema sahihi kuhusu Mwalimu. Kama kweli tunamuenzi tukumbuke jinsi alivyopigania ukombozi wa wanadamu wote bila kujali kabila, rangi, dini wala nchi
    Leo kuna wanatamka upuuzi kuwa eti hilo ni tataizo la Waarabu siye halituhusu. Mbona ukombozi wa Afrika Kusini, Angola n.k. uliungwa mkono kwa hali na mali na nchi kama China, Urusi, Sweden, Misri, Algeria, Cuba. Ni aibu kwa serikali yetu kujali zaidi misaada kuliko ubinadamu. Tumehongwa na Israel na kusahau ukaburu wao huko Palestina

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!