Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba aichambua Ripoti ya Hali ya Uchumi
Habari za Siasa

Prof. Lipumba aichambua Ripoti ya Hali ya Uchumi

Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF, ameichambua Ripoti ya Serikali ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2018, akisema kwamba baadhi ya takwimu zilizoanishwa katika ripoti hiyo haziendani na hali halisi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Prof. Lipumba ameeleza hayo leo tarehe 22 Juni 2019 katika Kongamano la Sauti ya Haki na Furaha kwa Wote lililoandaliwa na CUF na kufanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, Jijini Dar es Salaam.

Prof. Lipumba amesema  takwimu kuhusu ukuaji wa pato la taifa na la mwananchi haziendani na hali halisi ya uchumi wa nchi na wananchi, kutokana kwamba bado maisha ya Watanzania ni magumu na mazingira ya biashara kudorola.

“Hali yetu ya maisha hivi sasa imekuwa ni ngumu, wananchi wanalalamika wanasema vyuma vimekaza, ukisoma takwimu unaona takwimu nzuri. Lakini wafanyabiashara wanasema biashara haitoki. Moja ya tatizo mzungumko wa fedha katika uchumi umepungua,” amesema Prof. Lipumba.

Prof. Lipumba amesema kinachosababisha ugumu wa maisha ni ukosefu wa mazingira mazuri ya biashara pamoja na sera mbaya ya fedha zilizopelekea kudumaa kwa ukuaji uchumi na ujazi wa fedha.

“Ujazi wa fedha mwaka 2015 ulikuwa kwenye asilimia 14.5,  2016 ukapungua ukawa chini ya 1%, mwaka unaofuata ukawa kama 1.3%, mwaka jana ukawa chini ya 1%. Kwa wastani miaka mitatu iliyopita tokea 2016-2018 ujazi wa fedha za msingi, ukuaji wake uko chini ya 1%. Wakati hatuna tatizo la mfumuko wa bei,” amesema Prof. Lipumba na kuongeza.

 “Lazima patakuwa na tatizo katika mzungumko wa fedha. Utekelezaji wa sera yake ni nyepesi ni kiasi cha serikali iamue kukopa Benki Kuu, ujazi wa fedha utaongezeka.  Hili inawezekana.”

Kufuatia changamoto hizo, Prof. Lipumba ameishauri serikali kuziimarisha sekta binafsi, kuboresha sekta ya kilimo pamoja na kuwekeza katika nguvu kazi ya Watanzania.

“Ili kutoka tulipo lazima kuwekeza kwenye kilimo na viwanda. Lakini majukumu ya serikali ni kuwekeza kwenye nguvu kazi ya wananchi na kujenga mazingira ya sekta binafsi kuwekeza kwenye shughuli za biashara,” amesema Prof. Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

Habari za Siasa

ACT Wazalendo yaanika madudu miradi ya ujenzi, moundombinu

Spread the loveCHAMA cha ACT Wazalendo kimeeleza wasiwasi juu ya uelekeo wa...

Habari za Siasa

Samia ashuhudia utiaji saini ujenzi wa minara 758 ya bilioni 265

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa kampuni za...

error: Content is protected !!