Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Kabudi: Ni wivu tu
Habari za Siasa

Prof. Kabudi: Ni wivu tu

Spread the love

PROFESA Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amejigamba kwamba, kwenye nchi hii amefanya kazi ya kutukuka na kuwa, anayemchukia na kumwonea wivu, amchukie tu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

“Anayemchukia Kabudi na aendelee kumchukia, anayempinga na aendelee kumpinga, lakini Kabudi atabaki yule yule siku zote,” alisema.

Prof. Kabudi ambaye kitaaluma ni mwanasheria mbobezi alitoa kauli hiyo tarehe 30 Mei 2019 bungeni wakati akijibu hoja za wabunge katika mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2019/20.

Waziri huyo amesema kuwa, hatishwi wala kusononeshwa na wale wanaomtakia mabaya kwenye kazi yake na kuwa, uzalendo wake kwa taifa hili ni mkubwa na usiotiliwa shaka yoyote.

Akionekana kujibu mapigo kwa wale wanaombeza bila kuwataja, Prof. Kabudi alisema kuwa, yeye alisajiliwa katika dirisha dogo hivyo anayendelea kupiga hazi bila kuyumbishwa na watu wasiompenda ama kumtakia mema.

Prof. Kabudi aliwaeleza wabunge baadhi ya kazi alizozifanya kwa maslahi ya taifa, ikiwa ni pamoja na kuandaa na kuandika Sheria ya Mazingira ambayo inatumika mpaka hii leo.

Pia alieleza kuwa, ndiye aliyefanya kazi ya upatanishi kwa wabunge wa upinzani wakati huo, Hamad Rashidi Mohamed na Dk Wilbrod Slaa wakati wa kutunga sheria ya kupambana na rushwa.

Wakati akitoa kauli hiyo, alisoma Hansard (kumbukumbu rasmi) za Bunge zilizomtaja kwa wakati huo ili kuthibitisha kauli yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!