Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Posa ya CCM yahamia kwa Mbowe
Habari za SiasaTangulizi

Posa ya CCM yahamia kwa Mbowe

Spread the love

VUGUVUGU la madiwani wa upinzani kukimbilia Chama Cha Mapinduzi (CCM) halijapoa, jimboni Hai, Kilimanjaro katika Kata ya Kia, diwani wake amehamia chama tawala. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Timoth Laizer, ambaye alikuwa diwani wa kata hiyo kupitia Chadema sasa ni mwanachama wa CCM. Jimbo la Hai ndio linaongozwa na Freeman Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa.

Laizer leo tarehe Agosti 2, 2018 amesema kuwa, ameamua kuhama  Chadema kwa sababu alizozitaja kuwa ni kutoridhishwa na maelekezo yanayotolewa na uongozi wa chama hicho yakutoshiriki wala kutotambua kazi ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya CCM.

“Nimeamua kujiunga nha CCM chama pekee kilichobaki kuwatetea wanyonge katika nchi hii  kutokana na ukweli kwamba siwezi kuendelea kuwa kwenye chama kinachotupa maelekezo ya kutoshiriki wala kuzitambua kazi zozote zinazofanywa na Serikali wakati kiuhalisia serikali ya Rais John Magufuli ndio iliyoweza kupambana na shida na dhiki za watanzania wanyonge ” amesema Laizer.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mikataba ya utekelezaji bado haijasainiwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

error: Content is protected !!