Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi yawadaka wagombea wanaofuatilia rufaa NEC
Habari za Siasa

Polisi yawadaka wagombea wanaofuatilia rufaa NEC

Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma limewakamata wagombea ubunge na udiwani kutoka Chama cha Demokraaia na Maendeleo (Chadema) waliokuwa wanakwenda Ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) zilizopo Njedengwa Dodoma kufuatilia rufaa zao. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Polisi wamewakamata leo Jumamosi tarehe 5 Septemba 2020 wakiwa kwenye gari aina ya Haice eneo la Makulu majumba tatu baada ya kuwakuta askari polisi waliokuwa na silaha za moto huku wakiwa na gari lililokuwa na mbwa wa polisi.

Awali, gari hiyo iliyokuwa imewabeba wagombea hao pamoja na baadhi ya waandishi wa habari iliwafuata wabunge hao ofisi za Chadema Kanda ya Kati na kuanza safari ya kwenda ofisi za NEC.

Baadhi ya waliokamatwa na wako Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma ni kutoka majimbo ya Kilombero, Kilosa, Nzega Vijijini, Songea, Ukonga, Ludewa, Bahi pamoja na madiwani.

Kwa mujibu wa NEC, zaidi ya rufaa 550 zinakatwa na wagombea udiwani na ubunge ambazo wanazifanyia kazi.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!