Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi yaeleza sababu kumkamata kigogo BAVICHA
Habari za Siasa

Polisi yaeleza sababu kumkamata kigogo BAVICHA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno
Spread the love

 

JESHI la Polisi nchini Tanzania limetoa sababu ya kumshikilia Mratibu wa Uhamasishaji wa Baraza la Vijana Chadema (Bavicha), Twaha Mwaipaya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, Mwaipaya alikamatwa kwa tuhuma za kuchapisha katika mtandao wake wa twitter habari inazodai zilizua taharuki kwa umma.

Otieno ametoa sababu hizo leo Ijumaa, tarehe 8 Julai, 2022, akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema uchunguzi unaendelea na muda wowote atafikishwa mahakamani kusomewa mashitaka yake.

“Tunaendelea na uchunguzi na muda wowote tunatarajia kumfikisha Mahakamani kwa kosa la kutoa taarifa za uongo katika ukurasa wake wa Twiter,” amesema Otieno.

Mratibu wa uhamasishaji wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Twaha Mwaipaya

Amesema Mwaipaya alitoa habari hizo za uongo ikiwa yeye sio msemaji wa Serikali wala shirika la umeme nchini Tanzania (TANESCO).

“Serikali ina taratibu zake za kutoa taarifa zake rasmi msemaji wa Serikali yupo na kama ni Tanesco ambao wao wana mamlaka kutoa bei halisi za umeme,” amesema Kamanda Otieno na kuongeza

Itakumbukwa kuwa Mwaipaya alikamatwa tarehe 30, Juni, 2022 na kuachiwa kwa dhamana Jumanne tarehe 5, 2022, baada ya makada wenzake kupaza sauti na kufungua shauri mahakamani kutaka afikishwe mahakamni haraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!