Saturday , 2 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Polisi watoa ufafanuzi utata wa kifo cha mmiliki wa shule
Habari Mchanganyiko

Polisi watoa ufafanuzi utata wa kifo cha mmiliki wa shule

Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto
Spread the love

JESHI la polisi Mkoa wa Dodoma limetoa ufafanuzi juu ya kifo cha Ustadhi Rashid Ally Musa maarufu kwa jina la Rashid Ramadhani Bura (62). Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Jeshi la polisi limetoa ufafanuzi  kutokana na kutokea kwa utata na kauli mbalimbali ambazo zimeonekana kuichanganya jamii na wakazi wa Mkoa wa Dodoma kwa ujumla.

Kamada wa polisi Mkoa wa Dodoma ASCP Gilles Muroto, alisema kuwa jeshi la polisi lilibaini kuwa kifo cha Bura kilitokana na ugonjwa wa moyo.

Muroto alisema kuwa marehemu Bura ambaye ni Mkurugenzi wa Taasisi ya The Dalai Islamic Centre na Mmiliki wa shule ya Zamzam ambaye makazi yake yalikuwa Chang’ombe Extension jijini Dodoma alipatwa na mauti akiwa ofisini kwake kutokana na shinikizo la moyo.

Kamanda Muroto alisema kuwa kabla ya kifo chake tarehe 21 Desemba, 2019, alihudhuria Mkutano wa Mahusiano ya dini mbalimbali huko Jijini Dar es Salaam na kurejea Dodoma siku iliyofuata kwa kutumia usafiri wa basi namba T980 DNN la kampuni ya Kimbinyiko .

Alisema kuwa marehemu alikata tiketi namba 1947 na alipata siti namba 13 na baada ya kufika Dodoma alifikia ofisini kwake mtaa wa Barabara ya Nyerere, Kata ya Madukani Jijini Dodoma, na akiwa ofisini kwake alipatwa na tatizo la moyo na alizidiwa na kufariki dunia kwa kukosa msaada wa karibu.

“Kutokana na safari yake hiyo, alikosa mawasiliano na ndugu zake baada ya simu yake kuzima, na kwa kuwa ndugu walifahamu kuwa amesafiri, waliendelea kumtafuta kwa njia ya simu bila mafanikio, pia waliwasiliana na watu wengine aliokuwa nao katika safari hiyo hawakufanikiwa.

“Ilipofika tarehe 25 Desemba, mwaka huu, majira ya saa 11:00 jioni mtoto ake Ally Mussa alikwenda ofisini kwake na kukuta amefariki duniani na mwili wake ukiwa umevimba, unatoa harufu na umeharibika kutokana na kukaa takribani siku nne.

“Jeshi la polisi lilifika eneo la tukio na wataalam wa uchunguzi wa matukio kuchunguza tukio hilo, eneo la tukio ulifanyika uchunguzi na upekuzi katika ofisi yake na kugundua kuwa hakukuwa na uharibifu wowote katika ofisi yake, hakuna wizi wowote wa mali, upekuzi ulifanyika na lilikutwa begi dogo la nguo chacheza safari, simu yake ikiwa imezima, tiketi ya safari, Pesa katika pochi Sh. 260,000 na vitambulisho vyake.

“Mwili wa marehemu ulipelekwa hospitali ya Rufaa ya Dodoma na kufanyiwa uchunguzi na daktari kuthibitisha kuwa, kifo chake ni moyo kufeli na kushindwa kufanya kazi, hata hivyo jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma linaendelea kufanya uchunguzi kupitia simu zake kubaini kama kuna taarifa za ziada, na watu wasitumie taarifa ya kifo hiki kupotosha umma au kuunda taarifa zenye upotoshaji kama zinavyoenezwa mitandaoni,” alieleza Muroto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari Mchanganyiko

Waziri Bashungwa aagiza wahandisi kujengewa uwezo

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameiagiza Bodi ya Usajili wa...

Habari Mchanganyiko

Heche ataka mawakili vijana kuamka sakata Mpoki

Spread the loveMWENYEKITI wa Mawakili Vijana Tanzania kutoka Chama cha Mawakili wa...

error: Content is protected !!