Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi watanda makao makuu Chadema, wakamata wafuasi
Habari za Siasa

Polisi watanda makao makuu Chadema, wakamata wafuasi

Spread the love

JESHI  la polisi limewakamata watu kadhaa ambao walikuwa wakipita katika ofisi za makao makuu ya chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) zilizopo eneo la Ufipa, Kinondoni jijini Dar es salaam huku wakiwa wamevalia t shirt zilizoandikwa “Pray For Lissu”, anaandika Hellen Sisya.

Polisi hao ambao walikuja na magari yasiyopungua sita huku wakiwa na silaha, walizingira ofisi hizo kwa takribani masaa matatu kuanzia saa tisa mchana mpaka saa kumi na moja jioni hii huku wakihoji kila mtu ambaye alikuwa akifika katika ofisi hizo.

https://youtu.be/sZ9CI1nJs4Q

Mapema Leo hii  jeshi la polisi lilizingira viwanja vya Tip vilivyopo  eneo la Sinza, mahali ambapo chama hicho kilitarajiwa kufanya maombi kwa ajili ya mwanasheria mkuu Wa chama hicho Tundu Lissu ambaye anaendelea na matibabu nchini Kenya baada ya kushambuliwa kwa risasi wiki iliyopita mjini Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!