Monday , 29 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Polisi wanasa mtandao wizi wa magari ya umma
Habari Mchanganyiko

Polisi wanasa mtandao wizi wa magari ya umma

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu 15 wanaodaiwa kujihusisha na mtandao wa wizi wa magari,ikiwemo magari ya umma. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 6 Novemba 2018, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Liberatus Sabas amesema katika operesheni iliyofanywa na jeshi hilo, wamefanikiwa kukamata magari saba ikiwemo gari la wizara ya afya na la taasisi ya wanawake Tanzania.

Amesema katika watuhumiwa 15, mmoja wao aliyefahamika kwa jina la Dk. Yusuf Mwaipopo (42) alikamatwa na gari ya wizara ya afya.

“Natoa rai kwa madereva wa magari ya umma kwamba sehemu sahihi ya kupaki magari sio kwenye yadi za uchochoroni, magari ya umma yapaki kwenye ofisi za umma zenye ulinzi wa kutosha,” amesema Kamanda Sabas.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

Habari Mchanganyiko

Kampeni ya Samia Legal Aid yazinduliwa Manyara, kesi 45 zapokelewa

Spread the love  KAMPENI ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, imezinduliwa...

Habari Mchanganyiko

NMB ya kwanza kuzindua Malipo kwa QR na UnionPay International

Spread the loveBENKI ya NMB kwa kushirikiana na UnionPay International (UPI), wamezindua...

error: Content is protected !!