Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wamvaa Mbatia, aitwa kujieleza
Habari za Siasa

Polisi wamvaa Mbatia, aitwa kujieleza

James Mbatia, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi
Spread the love

ZIARA ya James Mbatia, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi imeingia shubiri mkoani Mbeya baada ya polisi kuvamia na kuzuia mkutano wake wa ndani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi … (endelea).

“Kwasasa naomba nisiseme chochote mpaka niitikie wito,” ameeleza Mbatia alipouliza kuhusu sababu za kuzuiliwa kufanya mkutano wake wa chama leo tarehe 5 Machi 2020.

Taarifa zaidi zinadai, Mbatia ameanza ziara kwenye eneo hilo kinyume na agizo la Rais John Magufuli, kwamba wabunge na madiwani wafanye siasa katika ameneo yao.

“Nikifika polisi na kuzungumza nao, ndio nitakuwa na nafasi nzuri ya kueleza,” amesisitza Mbatia wakati akitii agizo la kuzuia kwa mkutano wake akiwa katika Jimbo la Busokelo.

Polisi wilayani Ruangwa, Lindi hawajaeleza sababu za kuzuia mkutano huo, zaidi wamemtaka Mbatia kufika katika Kituo cha Polisi cha Lwangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!