JESHI la Polisi limemkamata Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na kuendelea kumshikiria hadi sasa pamoja na kuwa mgonjwa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Mdee alikamatwa leo alfariji akitokea Afrika Kusini alipokuwa amelezwa. Pamoja na daktari kuwathibitisha Polisi kuwa Mdee ni mgonjwa.
Polisi wanamshikiria Mdee wakitaka kumjumuisha katika kesi ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine watano ambao watafikishwa mahakamani kesho kutwa.
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA UMMA-KUKAMATWA KWA MHE. HALIMA MDEE (MB)
Leo Jumapili tarehe 01 Aprili 2018, majira ya saa tisa alfajiri Mhe. Halima Mdee (Mb) alikamatwa akiwa uwanja ndege wa Dar Es salaam alipokuwa amerejea nchini akitokea Nchini Afrika Kusini alipokuwa anapatiwa matibabu.
Mpaka mchana wa leo tarehe 01 Aprili, 2018 Jeshi la Polisi wameendelea kumshikilia Katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam na hajapatiwa dhamana pamoja na daktari wake kuwathibitishia polisi kuwa Mheshimiwa Halima ni mgonjwa.
Tunasikitishwa na kulaani kitendo hiki cha Polisi kuendelea kumshikilia mgonjwa ambaye alikuwa amelazwa hospitalini.
Tunatoa mwito kwa Jeshi la Polisi limpatie dhamana ili aweze kuendelea na matibabu yake, Kwani dhamana ni haki yake na zaidi ni kuwa huyu bado ni mtuhumiwa na ni Mgonjwa ambaye ametoka hospitalini.
Mwisho Jeshi la Polisi litawajibika kwa watanzania endapo afya ya Mhe. Halima Mdee ikitetereka au ikidhoofu zaidi na lawama zote zitakuwa juu yao.
Imetolewa Leo Jumapili tarehe 01 Aprili, 2018
John Mrema – Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje – CHADEMA
Leave a comment