Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wamng’ang’ania Mdee
Habari za Siasa

Polisi wamng’ang’ania Mdee

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera, bado linamshikilia Halima Mdee, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), tangu jana tarehe 14 Julai 2019. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kwa mujibu wa Tumaini Makene ambaye ni msemaji wa chama hicho, Mdee bado yupo mikononi mwa polisi kwa tuhuma za kufanya uchochezi.

Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe, jijini Dar es Salaam, Grace Tendega ambaye ni Katibu wa Bawacha, Conchesta Rwamlaza; Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Kagera na Anatropia Theonest; Mbunge Viti Maalum waliitwa katika Kituo cha Polisi cha Bukoba kuhojiwa.

Baada ya mahojiano hayo, ni Mdee pekee yake alinyimwa dhamana huku viongozi wengine wakiachwa.

“Polisi wanaendelea kumshikiria Mdee wakidai kuwa, wanasubiri maelekezo kutoka kwa Kamanda wa Mkoa wa Kagera aliyekuwa kwenye ziara ya Rais John Magufuli kwamba wamuachie kwa dhamana au wamfikishe mahakamani,” taarifa hiyo ya Chadema imeeleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!