Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wamng’ang’ania Mdee
Habari za Siasa

Polisi wamng’ang’ania Mdee

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera, bado linamshikilia Halima Mdee, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha), tangu jana tarehe 14 Julai 2019. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kwa mujibu wa Tumaini Makene ambaye ni msemaji wa chama hicho, Mdee bado yupo mikononi mwa polisi kwa tuhuma za kufanya uchochezi.

Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe, jijini Dar es Salaam, Grace Tendega ambaye ni Katibu wa Bawacha, Conchesta Rwamlaza; Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Kagera na Anatropia Theonest; Mbunge Viti Maalum waliitwa katika Kituo cha Polisi cha Bukoba kuhojiwa.

Baada ya mahojiano hayo, ni Mdee pekee yake alinyimwa dhamana huku viongozi wengine wakiachwa.

“Polisi wanaendelea kumshikiria Mdee wakidai kuwa, wanasubiri maelekezo kutoka kwa Kamanda wa Mkoa wa Kagera aliyekuwa kwenye ziara ya Rais John Magufuli kwamba wamuachie kwa dhamana au wamfikishe mahakamani,” taarifa hiyo ya Chadema imeeleza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!