Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Polisi wajichunguza tuhuma za kumpiga mwandishi
MichezoTangulizi

Polisi wajichunguza tuhuma za kumpiga mwandishi

Kamanda Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limesema linalaani vikali tukio linalosambaa mtandaoni la kupigwa kwa mwandiishi wa habari wa Wapo Radio aitwaye Sillas Mbise lililotokea August 08, 2018. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema Polisi Kanda Maalum imeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kufungua jalada la uchunguzi wa picha ya video hiyo inayosambaa inayoonesha askari wa Polisi na mwandishi huyo wa habari ili kubaini ukweli.

Mambosasa amesema hilo linaenda sambamba na kumtaka mtendewa wa kosa hilo la kupigwa kutoa taarifa kituo cha Polisi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwakuwa mtu yeyote anatakiwa kutoa malalamiko yake pale anapoona ametendewa vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria.

Sambamba na hayo Mambosasa amesema kuwa jukumu la Polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zao na si kuwapiga raia wakitenda kosa ambao hawajakataa kutii sheria ya kukamatwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!