JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limesema linalaani vikali tukio linalosambaa mtandaoni la kupigwa kwa mwandiishi wa habari wa Wapo Radio aitwaye Sillas Mbise lililotokea August 08, 2018. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema Polisi Kanda Maalum imeanza uchunguzi wa tukio hilo kwa kufungua jalada la uchunguzi wa picha ya video hiyo inayosambaa inayoonesha askari wa Polisi na mwandishi huyo wa habari ili kubaini ukweli.
Mambosasa amesema hilo linaenda sambamba na kumtaka mtendewa wa kosa hilo la kupigwa kutoa taarifa kituo cha Polisi ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwakuwa mtu yeyote anatakiwa kutoa malalamiko yake pale anapoona ametendewa vitendo ambavyo ni kinyume cha sheria.
Sambamba na hayo Mambosasa amesema kuwa jukumu la Polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zao na si kuwapiga raia wakitenda kosa ambao hawajakataa kutii sheria ya kukamatwa.
Leave a comment