Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wajichanganya, Bil 1.2 zawatokea puani
Habari Mchanganyiko

Polisi wajichanganya, Bil 1.2 zawatokea puani

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polsii Kanda Maalumu ya Dar es Salaam
Spread the love

ASKARI Polisi tisa wanashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kosa la kukiuka maadili ya kazi wakati wa ufuatiliaji wa sakata la wizi wa Sh. 1.2 bilioni uliofanywa na wafanyakazi wanne wa Kampuni ya Ulinzi ya G4S. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam…(endelea).

Pia, kanda hiyo inawashikilia wafanyakazi hao wa Kampuni ya G4S kwa tuhuma za wizi wa Sh. 1.2 bilioni, Dola za Marekani 402,000 na Euro 27,700, mali ya Benki ya NBC.

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2020 na SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polsii Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, wakati akizungumza na wanahabari.

Kamanda Mambosasa amewataja watuhumiwa hao kuwa ni, Christopher Rugemalila (34) ambaye alikuwa dereva wa G4S, mkazi wa Chanika, Mohamedi Ramadhani( 40) mkazi wa Mtoni Kijichi, Salimu Shamte (45) mkazi wa Mbagala Kizuiani, Ibrahimu Maunga (49), Mkazi wa Kiluvya.

Kamanda Mambosasa amedai kuwa, watuhumiwa hao walitekeleza uhalifu huo tarehe 7 Februari 2020, baada ya kutokomea kusikojulikana na fedha hizo ambazo walielekezwa kuzipeleka makao makuu ya Benki ya NC yaliyoko Posta ya zamani.

Akifafanua zaidi kuhusu tukio hilo, Kamanda Mambosasa amesema watuhumiwa hao walitelekeza gari ya kampuni ya 4GS iliyokuwa imebeba fedha hizo, baada ya kuzihamishia katika gari binafsi iliyokuwa inaendeshwa na Salumu Shamte.

“Walinzi hao walikabidhiwa fedha kutoka tawi la benki ya NBC Kariakoo na Samora ili wazipeleke makao makuu, lakini hawakufanya hivyo, matokeo yake walipanga njama na kuelekea maeneo ya Temeke Maduka Mawili karibu na kituo cha mafuta cha Camel,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amesema baada ya uhalifu huo kutokea, Jeshi la Polisi liliunda kikosi kazi kilichofuatilia watuhumiwa hao na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa wa kwanza ambaye ni Regemalila, aliyekamatwa tarehe 17 Februari 2020 maeneo ya Mongo la Ndege.

“Rugemalila alikamatwa na alipopekuliwa alikutwa na Tsh. 110,000,000, Dola 19,000 zikiwa ndani ya gari lake na magari matano. Baada ya kuhojiwa alikiri kuchukua fedha hizo na kusema kwamba amenunua nyumba mbili na kiwanja kimoja vyenye thamani ya 107,000,000,” amesema Kamanda Mambosasa na kuongeza.

“Tarehe 21 watuhumiwa wawili walikamatwa (Mohamedi na Salimu) maeneo ya Mbagala, na walipopekuliwa walikutwa na Tsh. 332,000,000, Dola za Mareknani 50,000, Euro 5010 na gari iliyotumika kubebea fedha.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!