Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Michezo Polisi Tanzania yatoa sababu kuendelea kumshikilia Idris
Michezo

Polisi Tanzania yatoa sababu kuendelea kumshikilia Idris

Idriss Sultan
Spread the love

JESHI la Polisi nchini Tanzania, limeeleza sababu za kuendelea kumshikilia Idris Sultani, Msanii wa Vichekesho Tanzania, anayesota rumande kwa muda wa siku tano, ni uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili kutokamilika. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Idris anashikiliwa katika Kituo  cha Polisi cha Oysterbay, wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, tangu tarehe 19 Mei 2020, alipojisalimisha kituoni hapo, kwa ajili ya kuhojiwa dhidi ya kosa la uonevu kwa njia ya mtandao, linalomkabili.

Msanii huyo amekumbwa na tuhuma hizo, baada ya video inayomuonesha akiicheka picha ya zamani ya Rais John Magufuli, kusambaa mitandaoni hivi karibuni.

David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, akizungumza na Mwanahalisi Online kwa  simu, leo Jumamosi tarehe 23 Mei 2020, amesema msanii huyo hajapewa dhamana kwa kuwa, uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili haujakamilika.

Misime amesema, Jeshi la Polisi haliwezi kukimbilia kumpa mtuhumiwa dhamana, wakati uchunguzi wa tuhuma zake haujakamilika.

“Kwanza niseme kwamba, ukikamatwa na polisi kwa tuhuma fulani wakati wa kukusanya ushahidi, wakati tunakuhoji tukigundua una makosa mengine tutaendelea kukuhoji nayo.  Hatuwezi kukimbilia kukupa dhamana eti kwa sababu kuna dhamana,” amesema Misime

“Lazima tukamilishe haya ambayo tunaona kwamba kuna umuhimu wa kufanya uchunguzi wa kutosheleza, ili kama mtu anapoonekana kuna  ushaidi wa kupelekwa mahakamani, apelekwe mahakamani na kama hakuna ushaidi aweze kuachiwa.”

Mapema leo Jumamosi asubuhi, wakati akizungumza na Mwanahalisi Online kwa njia ya simu leo, Benedict Ishabakaki, Wakili wa Idris, amesema anaendelea kufuatilia dhamana ya msanii huyo.

“Jana walikataa kutoa dhamana, na hawajatoa sababu. Wakishakwambia hakuna dhamana ina maana kesho yake unafuatilia tena, hivyo leo nafuatilia dhamana maana wanatoa siku yoyote,” amesema Wakili Ishabakaki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

error: Content is protected !!