JESHI la Polisi Tanzania limesema, Kiongozi wa Kanisa la Efatha, Mtume na Nabii Josephat Mwingira alikwisha kufika na kuandika maelezo juu ya tuhuma alizozitoa dhidi ya Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa aliyoitoa leo Ijumaa, tarehe 30 Desemba 2021, Msemaji wa Jeshi hilo, David Misime, “Askofu Mwingira alishafika polisi na kuandika maelezo yake.”
“Hatua zinazoendelea tangu atoe maelezo hayo ni kufanyika kwa uchunguzi wa aliyoyaeleza,” ameongeza Misime.
Hata hivyo, taarifa hiyo haikufafanua Nabii Mwingira alihojiwa linin a wapi na kwa maelezo ya awali, nini wamekibaini.
Nabii Mwingira anatuhumiwa kutoa tuhuma nzito za kunusurika kuuawa mara tatu na watu wa serikali jambo lililomfanya Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene kuagiza Polisi kumtafuta na kumhoji kuhusu tuhuma hizo.
Leave a comment