Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar yapiga ‘stop’ disko toto
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar yapiga ‘stop’ disko toto

Dk. Lazaro Mambosasa
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, limepiga marufuku disko toto katika kumbi zote za starehe mkoani humo, wakati wa sherehe za sikukuu ya Eid El-fitri. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Jeshi hilo kwa kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, vimejipanga kikamilifu kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu hiyo inayotarajiwa kuadhimishwa kesho au keshokutwa Ijumaa, tarehe 14 Mei 2021.

Hayo yamesemwa leo Jumatano, tarehe 12 Mei 2021 na Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema, wamejipanga kuimarisha doria maeneo yote muhimu zikiwemo nyumba za ibada, fukwe za bahari, kumbi za starehe na maeneo mengine yote yatakayokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha wananchi wote wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu.

Pia, wazazi wahakikishe watoto wao hawatembei peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu na kutowaruhusu kuogelea peke yao, kitendo ambacho kinaweza kuzuia watoto hao kuzama kwenye maji.

“Wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo,” amesema

Mambosasa, amewataka madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoendesha magari au pikipiki wakiwa wametumia vilevi/pombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!