Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Polisi Dar yapiga ‘stop’ disko toto
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar yapiga ‘stop’ disko toto

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

 

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, limepiga marufuku disko toto katika kumbi zote za starehe mkoani humo, wakati wa sherehe za sikukuu ya Eid El-fitri. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Jeshi hilo kwa kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, vimejipanga kikamilifu kuimarisha usalama katika kipindi cha sikukuu hiyo inayotarajiwa kuadhimishwa kesho au keshokutwa Ijumaa, tarehe 14 Mei 2021.

Hayo yamesemwa leo Jumatano, tarehe 12 Mei 2021 na Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa, wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema, wamejipanga kuimarisha doria maeneo yote muhimu zikiwemo nyumba za ibada, fukwe za bahari, kumbi za starehe na maeneo mengine yote yatakayokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha wananchi wote wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu.

Pia, wazazi wahakikishe watoto wao hawatembei peke yao bila ya kuwa na uangalizi wa karibu na kutowaruhusu kuogelea peke yao, kitendo ambacho kinaweza kuzuia watoto hao kuzama kwenye maji.

“Wamiliki wa kumbi za starehe wanatakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa kumbi hizo,” amesema

Mambosasa, amewataka madereva wa vyombo vya moto wanatakiwa kuendelea kufuata sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na kutoendesha magari au pikipiki wakiwa wametumia vilevi/pombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!