Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar wamsaka mume aliyemuua mke
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar wamsaka mume aliyemuua mke

Jumanne Muliro, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

 

GODBLES Sawe, mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam, anatafutwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kwa tuhuma za kumuua mkewe, Ester Benito Gadau, kwa kumkata kwa kitu chenye ncha kali kichwani, kisha kutokomea kusikojulikana. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Alhamisi, tarehe 16 Juni 2022 na Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, ACP Jumanne Muliro, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Kamanda Muliro amesema, mtuhumiwa alitekeleza tukio hilo tarehe 14 Juni 2022, maeneo ya Kibamba.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, linamtafuta Godbles Sawe, miaka 47, Mchaga, fundi Friji mkazi wa Kimara Suka, kwa tuhuma za kumuua mke wake Ester Benito Gadau, kwa kumkata kwa kitu chenye ncha kali kichwani huko maeneo ya Kibamba, Wilaya ya Ubungo na kukimbia baada ya kutekeleza mauaji hayo,” amesema Kamanda Muliro.

Katika hatua nyingine, Kamanda Muliro amesema, wamemfikisha mahakamani Joshua Simangwe, kwa tuhuma za kuwalawiti watoto watatu, ambao ni wanafunzi.

“Kesi kadhaa zimetolewa taarifa kwenye vituo vya Polisi, mkazo maalum umewekwa ili kesi hizi zipelelezwe haraka na baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa mahakamani akiwemo Joshua Simangwe, miaka 66, mkazi wa Kipunguni Ukonga anayetuhumiwa kuwalawiti watoto watatu wenye umri chini ya miaka 18 ambao ni wanafunzi huko maeneo ya Gongolamboto Dar es salaam,” amesema Kamanda Muliro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!