Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi afumwa na bangi, gongo, viroba
Habari Mchanganyiko

Polisi afumwa na bangi, gongo, viroba

Spread the love

JESHI la Polisi nchini Tanzania, limemtimua kazi ofisa wake kwa kukutwa na bangi, gongo, viroba pamoja na kujiunganishia umeme kinyume cha utaratibu. Anaandika Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Polisi huyo aliyetambulika kwa jina la F.1445 Koplo William, alifukuzwa baada ya Kenan Kihongosi, Mkuu wa Wilaya ya Arusha kuvamia nyumbani kwa askari huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi tarehe 7 Januari 2021, Salum Hamduni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha amesema, Kihongosi alivamia nyumbani kwa askari wake baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi.
Kamanda huyo amesema, mkuu huyo wa wilaya na timu yake walipofika nyumbani kwa Koplo William, miongoni mwa mambo waliyobaini ni pamoja na kujiunganishia umeme kinume cha sheria.

Salumu Hamduni, RPC Arusha

Pia, walikuta mafuta ya dizeli lita 85, gongo lita tano, misokoto ya bangi 20 na viroba vilivyokatazwa na serikali boksi 84 ambavyo vimekatazwa na serikali pia chupa zenye konyagi tisa.

Amesema, uvamizi huo ulifanywa tarehe 5 Januari 2021, saa tatu usiku katika Mtaa wa Muriet, Kata ya Sokoni One.

Kamanda Hamduni amesema, askari wengine watatu walikamatwa kwa tuhuma za rushwa baada ya kushawishi kutaka rushwa kutoka kwa Sammy Mollel, mmiliki wa Kampuni ya Gems and Rocks Venture.

Na kwamba, askari hao walimteka Lucas Mdeme, Meneja wa Kampuni ya kuuza madini ya Crown Lapidary, Arusha wakimtaka awape Sh. 30 milioni.

Askari waliohusika katika tukio hilo ni Gasper Paul (H.125) kutoka Kitengo cha Intelijensia Makao Makuu, Heavenlight Mushi (G.5134) kutoka Kitengo cha Intelijensia Mkoa wa Kinondoni na Bryton Murumbe (H.1021) aliyekuwa Polisi Kazi za Kawaida Dodoma.

Kamanda Hamduni amesema, upelelezi wa kesi zao umekamilika na sasa, majalada yao yanapelekwa kwenye ngazi nyingine kwa hatua zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!