MIZENGO Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya Tatu ya Chuo cha Uuguzi (DECCA), yatakayofanyika tarehe 13 Desemba 2019, katika Kampasi ya Nala, Jijini Dodoma. Anaripoti Dandon Kaijage, Dodoma…(endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari, Hilda Mgimba ambaye ni Ofisa Utawala wa chuo hicho, amesema decca kinatarajia kuwatunukia vyeti na diploma ya uuguzi wahitimu 588.
Amesema, chuo hicho kimekuwa kikitoa masomo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mambo ya maabara, utabibu na ufamasia, ukunga na uuguzi.
Hilda ameeleza, chuo kimekuwa kikijitahidi kuhakikisha kinafundisha wanachuo kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi na ueledi mkubwa.
Leave a comment