Friday , 29 March 2024
Habari za Siasa

Pigo lingine Chadema

Edward Sembeye, Mkuu wa Mawasiliano ya Umma NCCR-Mageuzi
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinaendelea kukimbiwa na baadhi ya makada wake muhimu, tena waliokuwa na mamlaka. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Edward Sembeye, aliyekuwa Katibu wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), leo tarehe 26 Februari 2020, ametangaza kujitenga na chama hicho na kwamba anapumzika siasa.

Mbele ya waandishi wa habari, Sembeye amesema moja ya vitu vinavyokiumiza chama hicho, ni chama hicho kwenda ama kuendeshwa kwa mdundo wa Freeman Mbowe, mwenyekiti wa chama hicho na si Katiba ya Chadema.

“Leo mambo ya Chadema yanaamuliwa kwa mujibu wa kauli na amri za Mbowe (Freeman Mbowe), sio Katiba. Mwenyekiti ameamua kugeuzi chama kuwa mali yake binafsi.

“Lakini tukitoka nje tunawaaminisha umma wa Watanzania kwamba chama hiki ni mali ya Watanzania. Kuna mambo mengine kiuongozi, tunapaswa kuwa na akiba ya maneno,” amesema.

Amesema, kutokana na kutokuwa na umoja na msimamo, matokeo yake wamepoteza hata majiji waliyokuwa wakiyaongoza.

“…tumechukua Jiji la Dar es Salaam, tumechukua Jiji la Arusha, leo tumeyapoteza majiji yote na bado tunawaambia Watanzania kuwa bado tupo imara,…” amesema.  

Sembeya ameonesha kukerwa na maneno ya kejeli yanayotolewa na viongozi wa Chadema pia wajumbe wa Kamati Kuu, akisema jambo hilo si la kistaarabu.

“Juzi nimeona mjumbe mmoja wa Kamati Kuu akisema yule aliyehama ni panya,…

“Dhumuni la chama chetu ni kutetea haki za binadamu, kumwita mtu panya kwa sababu ameondoka kwenye chama chako! Kuna watu wameitwa wanaume suruali, mtu huyu ni Mjumbe wa Kamati Kuu,” amesema.  

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!