Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Picha ya JPM yamwingiza matatani Idriss Sultan
Habari za Siasa

Picha ya JPM yamwingiza matatani Idriss Sultan

Idriss Sultan
Spread the love

PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, amemuagiza Mchekeshaji Idris Sultan, kuripoti katika Kituo cha Polisi, kwa madai kwamba amevuka mipaka yake ya kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Makonda ametoa agizo hilo leo tarehe 30 Oktoba 2019, kupitia ukurasa wake wa Instagram, nusu saa baada ya Idris kuandika ujumbe ulioambatana na picha ya Rais John Magufuli, iliyohaririwa.

“Naona mipaka ya kazi yako huijui. Nenda sasa hivi kituo chochote cha polisi uwambie Makonda kaniambia nije, utakuta ujumbe wako,” ameagiza Makonda.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Idris aliandika ujumbe ulioambatana na picha ya Rais Magufuli, akisema kwamba “kwa siku moja tukabadilishana kazi ili a-enjoy birthday yake kwa amani.”

Mchekeshaji huyo ameandika ujumbe huo, ikiwa ni siku moja baada ya Rais Magufuli kusheherekea kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!