Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Penzi la Kajala, Harmonize lavunjika tena!
Michezo

Penzi la Kajala, Harmonize lavunjika tena!

Spread the love

YAMKINI uhusiano kati ya Msanii wa Bongo Muvi, Kajala Masanja na wa Bongofleva Rajabu Abdul ‘Harmonize’, umevunjika.

Hatua hiyo inakuja baada ya jana tarehe 8 Disemba, 2022 Kajala kuchapisha ujumbe kwenye akaunti yake ya Instagram unaoashiria kuwa wawili hao hawapo pamoja tena. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kajala ameandika hivi, “Mimi kama mwanamke na binadamu nimeumbwa kupenda na kusamehe pia, ila kwenye hili nastahili kuchekwa, nastahili kubezwa na kudharauliwa pia.

“Sipo hapa kujitetea wala kutia huruma ni kweli nilifanya makosa na nimeyagundua makosa yangu, mimi siyo mkamilifu. Hakika nimekosea familia yangu, ndugu zangu, na marafiki zangu. Kutenda kosa si kosa, kosa kurudia kosa. I forgive my X and I’m ready for the next.#Nimekoma# emporary post” – @kajalafrida.
Ujumbe huo umezidi kuzua mjadala katika mitandao ya kijamii hasa ikizingatiwa Juni 25 mwaka huu, Harmonize alimvalisha pete Kajala.

Tukio hilo lililopewa jina la ‘Late lunch’ lilihudhuriwa na watu wachache ambao ni marafiki na ndugu wa wasanii hao.

Aidha, Harmonize alifikia hatua hiyo baada ya kuhaha kwa zaidi ya miezi kadhaa ya kumuomba msamaha Kajala ikiwamo kumnunulia magari mawili ya Range Rover pamoja na kubandika picha yake kwenye mbao za matangazo katika barabara kubwa.

Hata hivyo, kabla ya penzi lao kurejea upya, wawili hao walitengana baada ya kudumu kwenye uhusiano wa kwanza kwa muda wa miezi miwili kuanzia Februari hadi Aprili mwaka jana.

Tukio hilo lilizua taharuki baada ya Harmonize kuwashtaki Kajala na mwanaye Paula kwamba wamevujisha picha zake za utupu kutokana na madai ya Mkurugenzi huyo wa Konde Boy kumshawishi Paula ili wabanjuke kimapenzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!