Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Michezo Payet amvuruga kocha wake
Michezo

Payet amvuruga kocha wake

Dimit Payet
Spread the love

KOCHA wa West Ham United Slaven Bilic, amesema winga wa klabu hiyo Dimit Payet 29 amekataa kucheza tena kwenye timu hiyo, kutokana na shinikizo la kutaka kuuzwa ingawa hawapo tayari kumuachia mchezaji huyo kwa sasa.

Payet ambaye alinunuliwa kutoka klabu ya Olympic Marseille inayo shiriki ligi nchini Ufaransa, kwa ada ya uhamisho Pauni Milioni 10 katika dirisha kubwa la usajiri amekuwa na mchango mkubwa ndani ya timu hiyo katika msimu uliomalizika kiasi cha kuvutia klabu kubwa barani Ulaya kutaka kumsajili.

Licha ya kugoma kucheza kwa sasa, lakini Bilic amesema hawako tayari kumuuza mchezaji huyo katika kipindi hiki ingawa haitaji kucheza hapo kwa sasa.

“Tumeshasema hatuitaji kumuuza mchezaji wetu bora kwa sasa, lakini Payet hataki kucheza kwetu” amesema Bilic

Katika msimu wa kwanza aliocheza akiwa na West Ham United, Payet alifunga jumla ya mabao 12 na kuchaguliwa kuwania tuzo za mchezaji bora wa kulipwa wa mwaka, nchini England.

West Ham ambayo mpaka sasa inashika nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi kuu nchini England, inatarajia kuwakalibisha Crystal Palace katika mchezo wa ligi siku ya Jumamosi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

error: Content is protected !!