Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Papa Francis ateua maaskofu wawili Dar
Habari Mchanganyiko

Papa Francis ateua maaskofu wawili Dar

Spread the love

 

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amewateua mapadre, Henry Mchamungu na Stephano Musomba, kuwa Maaskofu wasaidizi Jimbo Kuu la Dar es Salaam, nchini Tanzania. Anaripoti Ibrahim Yamola…(endelea).

Uteuzi huo, umetangazwa leo Jumatano, tarehe 7 Julai 2021 na Askofu Mkuu, Jude Thaddeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, katika misa takatifu ya upadrisho kwa mapadre 14, iliyofanyika viwanja vya Msimbazi Center.

Mara baada ya kumaliza kuwapa daraja hilo takatifu, Askofu Mkuu Rwa’ichi alisema Baba Mtakatifu, Francis amewateua Mapadre Mchamungu na Musomba kuwa maaskofu wasaidizi.

Kisha Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Charles Kitima akatoa taarifa rasmi ya uteuzi huo akisema, Askofu mteule, Mchamungu, alizaliwa tarehe 18 Januari 1965, Legho Kilema, jimbo la Moshi, Kilimanjaro.

Amesema, baada ya masomo yake ya upadre, alipewa daraja takatifu la upadre tarehe 24 Juni 1994 na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za utume Jimbo Kuu la Dar es Salaam na TEC.

Hadi anateuliwa kuwa Askofu mteule, Mchamungu alikuwa Mwalimu na mlezi wa seminari ya Segerea, Dar es Salaam.

Padre Kitima amesema, Askofu mteule Musomba, alizaliwa tarehe 25 Septemba 1969, Malonji Jimbo la Mbeya.

Baada ya masomo ya upadre, alipewa daraja takatifu la upadre tarehe 24 Juni 2004 na kuhudumu katika nafasi mbalimbali za uteme shirikani na Jimbo Kuu la Dar es Salaam na Morogoro.

Hadi uteuzi wake, Askofu mteule Musomba alikuwa Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mkingiwa Dhambi ya Asili- Mavurunza, Dar es salaam na Katibu wa Shirika lake la Waangustiniani Kanda ya Tanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!