Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Papa Francis ‘amtimua’ Pompeo
Habari

Papa Francis ‘amtimua’ Pompeo

Spread the love

MIKE Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amegomewa kukutana na Papa Francis, Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Dunani. Inaripoti Shirika la Habari la Uingereza (BBC)…endelea.

Hatua hiyo inatokana na msimamo wa Papa Francis kueleza kwamba, katika kipindi hiki cha kampeni za Marekani, kiongozi huyo hatokutana na mwanasiasa yeyote.

Waziri huyo inaelezwa, alitaka kwenda kuonana na Papa Francis ‘kuweka sawa mambo’ baada ya kutoa kauli iliyokasirisha Vatcan kwamba, kanisa hilo linapoteza mamlaka yake ya kinidhamu kwa kufanya makubaliano mapya na China kuhusu uteuzi wa maaskofu.

Na kwamba, mgogoro wa kidiplomasia kati ya China na Marekani ndio uliomsukuma Pompeo kutaka kuitumbukiza Vatcan na kulichafua kanisa hilo mbele ya uso wa dunia.

Vatican imemkatalia waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Mike Pompeo kuonana na Papa Francis.

Kiongozi huyo wa juu wa Kanisa Katoliki ameelezwa hawapokei wanasiasa wakati wa kipindi cha uchaguzi.

Hatua hiyo inaongeza hali ya mzozo wa kidiplomasia baada ya kauli ya Pompeo kuhusu China na Kanisa Katoliki.

Mwaka 2018 Vatican ilifanya makubaliano na China kuwa na maoni juu ya uteuzi wa maaskofu wa China.

Wakati huo huo, Papa Francis alisema, mpango huo utaponya vidonda vya zamani na kuleta umoja kamili wa Kikatoliki nchini China.

Makundi ya haki za binadamu yamekuwa yakieleza kwamba, Wakatoliki wengi nchini China, wanateswa kwa kuahidi utii kwa Papa badala ya chama rasmi cha Wakatoliki nchini China.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Habari

Tanzania yaungana na nchi 180 kushiriki maonesho ya utalii Ujerumani

Spread the love  TANZANIA imeungana na mataifa 180 duniani kushiriki maonesho makubwa...

ElimuHabari

NACTVET yatoa tuzo kwa wanaotoa nafasi kuendeleza ujuzi,Majaliwa ataka uwekezaji kwenye rasilimali watu

Spread the love BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTIVET) kwa...

error: Content is protected !!