Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Papa Francis ambusu miguu Salvar Kiir, ataka aache mapigano
Habari Mchanganyiko

Papa Francis ambusu miguu Salvar Kiir, ataka aache mapigano

Spread the love

KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis amempigia magoti Rais wa Sudani Kusini, Salvar Kiir akimsihi kiongozi huyo kuachana na mapigano katika taifa lake. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Papa Francis amefanya tukio hilo jana tarehe 11 Aprili 2019 alipokutana na Rais Salvar Kiir pamoja na Mpinzani wake Riek Machar, mjini Vatcan.

Kwa mujibu wa video uliyosambazwa katika vyombo vya habari vya kimataifa, inamuonesha Papa Francis akiwabusu miguuni wanasiasa hao, kama ishara ya kuwasihi kuachana na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe na kudumisha amani nchini Sudan Kusini.

Salva Kiir aliingia madarakani tangu Sudani Kusini ilipopata uhuru mwaka 2011, kisha mwaka 2013 vita vya wenyewe kwa wenyewe vilizuka nchini humo, vilivyosababishwa na uhasama kati ya Rais Kiir na Machar ambaye alikuwa na mikakati ya kumrithi.

Mnamo mwezi Julai mwaka  jana, Rais Kiir aliingia mkataba wa amani na mpinzani wake Riek Machar, ambapo wote kwa pamoja walikubaliana kusitisha mapigano ya wenyewe.

Attachments area

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!