KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano amelazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu baada ya kukabiliwa na matatizo ya kupumua katika siku za hivi karibuni. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Msemaji wa Vatican, Matteo Bruni amesema kwamba Papa mwenye umri wa miaka 86 hana Covid 19.
Aidha, amesema Papa Francis atakaa hospitali kwa siku kadhaa za matibabu.
Hii ni mara ya kwanza kwa Francis kulazwa hospitali tangu alipokaa siku 10 katika hospitali ya Gemelli mwezi Julai mwaka wa 2021 na kufanyiwa upasuaji kwenye tumbo.
Maswali yameibuka kuhusu hali ya afya ya Francis na uwezo wake kusherehekea matukio mengi ya wiki takatifu ambayo inaanza mwishoni mwa wiki hii na Jumapili ya matawi.
TBC, TB, TBS, TIB BANK, TBL inawakaribisha wenye mashindano ya mapinduzi (work on talk “mapinduzi”) ya BANGO la Vifo VYA TB, kudhibitisha viwango vya Tabia, uhifadhi wa fedha bank, UJENZI wa BAR nchini Tanzania MTAWALIA