Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Palestina ‘yatua’ ICC, yaituhumu Israel
Kimataifa

Palestina ‘yatua’ ICC, yaituhumu Israel

Spread the love

 

SERIKALI ya Palestina, imeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), iwachunguze maafisa wa Serikali ya Israel wanaotuhumiwa kufanya vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya raia wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa na Ubalozi wa Palestina nchini Tanzania baada ya Ripoti ya Shirika la Haki za Binadamu la Human Rights Watch (HRW), kubainisha vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyodaiwa kufanywa na baadhi ya maafisa wa Serikali ya Israel.

“Ubalozi wa Palestina unapenda kutoa msimamo wa Serikali ya Palestina kukaribisha ripoti ya HRW, juu ya uhalifu wa Israeli dhidi ya ubinadamu, ubaguzi wa rangi na mateso, ikiitaka ICC ichunguze maafisa wa Israeli wanaohusishwa na uhalifu huu,” imesema taarifa ya Ubalozi wa Palestina.

Taarifa ya ubalozi huo imesema, Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina, imesema vitendo hivyo vinavyofanywa na utawala wa Israel vinaathiri maisha ya Wapalestina, hasa kufuatia hatua yake ya kuendelea kuchuku ardhi ya Taifa hilo.

“Ripoti hiyo imefichua hali ya ukoloni wa Israeli kama serikali iliyokita mizizi ya ukuu wa Kiyahudi na utawala juu ya watu wa Palestina na uongezekaji wa makazi haramu katika eneo la Palestina na hivyobasi kuathiri kila sehemu ya maisha ya Wapalestina,” imesema Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina.

Kufuatia vitendo hivyo, Ubalozi wa Palestina nchini Tanzania, umezitaka Jumuiya za Kimataifa kuingilia kati vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu, vinavyofanywa na utawala wa Israel dhidi ya raia wa Taifa hilo.

“Ubalozi pia unakumbusha Mataifa na viongozi wa mataifa mbalimbali kuwa uhalifu wa ubaguzi wa rangi ni tishio kubwa kwa amani na usalama wa kimataifa.  Hivyo basi, mataifa na jamii ya kimataifa lazima ichukue hatua za haraka na madhubuti kulazimisha kukomeshwa kwa utawala wa kibaguzi wa Israeli,” imesema taarifa ya ubalozi huo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Serikali ya Israel inatuhumiwa kukandamiza mifumo ya uongozi wa Wapalestina, pamoja na kuzuia harakati zao za kudai ardhi yao iliyotwaliwa na Waisrael.

Ripoti ya HRW imekuja miezi mitatu baada ya kuchapishwa kwa ripoti ya Shirika la Haki za Binadamu la Israeli (B’Tselem), ambayo pia iliishutumu Israeli kuwa serikali ya ubaguzi wa rangi na isiyofuata misingiya kidemokrasia kama inavyojinasibu ulimwenguni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!