Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Padre Kitima awashukia viongozi dini wanaofumbia macho dhambi za uchaguzi
Habari za Siasa

Padre Kitima awashukia viongozi dini wanaofumbia macho dhambi za uchaguzi

Wapiga kura
Spread the love

KATIBU Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Padre Charles Kitima amewataka viongozi wa dini kukemea dhambi zinazojitokeza katika chaguzi, ili kuhakikisha zinakuwa za haki. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Padre Kitima ametoa wito huo leo tarehe 17 Novemba 2023, akitoa mrejesho wa ziara ya baadhi ya viongozi wa dini kwenda kujifunza namna ya kutenda haki kwenye uchaguzi, katika nchi zilizofanikiwa katika masuala hayo, ikiwemo Kenya na Afrika Kusini.

Kiongozi huyo wa dini amedai kuwa, imefika mahali baadhi ya viongozi wa dini wanaona makosa au dhambi zinazofanyika katika chaguzi, kama sio chukizo mbele za Mungu.

Padri Charles Kitima

“Na kwenye uchaguzi Tanzania imefika mahali viongozi wa dini sijui kama mtalionaje, ni kama dhana ya dhambi inafutwa kabisa kwenye mambo ya siasa. Yaani unaweza kufanya tendo ambalo si zuri kwenye siasa na ikaonekana si dhambi havimchukizi Mungu,” amesema Padre Kitima.

Akizungumzia ziara ya viongizi wa dini nchini Kenya, Padre Kitima amesema walifanikiwa kujifunza masuala mbalimbali ambayo amedai hapa hayapo, ikiwemo tume ya uchaguzi nchini humo kuaminika mbele ya wananchi, kutenda haki kwa wagombea wa pande zote, pamoja na kuwaandaa wananchi kushiriki uchaguzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

error: Content is protected !!