Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Pablo amgalagaza Nabi
HabariMichezo

Pablo amgalagaza Nabi

Spread the love

 

KOCHA wa klabu ya Simba Pablo Franco amechaguliwa kuwa kocha bora wa LigI Kuu Tanzania Bara mwezi Machi mara baada ya kumshinda kocha wa Yanga Mohammed Nasredine Nabi pamoja na Francis Balaza wa Kagera Sugar ambao aliingia nao fainali. Anaripoti kelvin Mwaipungu…(endelea)

Pablo ameshida tuzo hiyo mara baada ya kuchaguliwa na kamati ya tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania ‘TFF’ iliyokaa hivi karibuni.

Katika michezo waliocheza Simba ndani ya mwezi Machi, ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-0, dhidi ya Biashara United na pia ikaifunga Dodoma jiji mabao 2-0.

Kocha huyo alijiunga na Simba mwanzoni mwa msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2021/22, kwa kurithi mikoba ya Didier Gomes ambaye aliamua kuachana na timu hiyo kufutaia kupata matokeo mabaya kwenye Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.

Pablo anakuwa kocha wa sita kuzoa tuzo hiyo ya mwezi, toka kuanza kwa msimu huu huku makocha wengine waliotwaa tuzo hiyo ni Nabi ambaye alitwaa mara mbili mwezi wa Februari na Oktoba, Baraza mwezi Januari, Salum Mayanga Novemba, Malale Hamisi mwezi Septemba na Melis medo aliyekuwa anakinoa kikosi cha Coastal Union ambaye alitwaa tuzo hiyo Desemba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!