MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa ameshatumiwa majina ya wanaume 100 wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja na jumbe 5,763. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Kupitia taarifa yake Makonda ameeleza kuwa wanaDar es Salaam wamewachoka na hawapendezwi na tabia ya ushoga hivyo wametoa ushirikiano na ofisi yake.
Zoezi hilo limeibuka mara baada ya msanii wa muziki wa kizazi kipya Amber Rutty kuachia video yake ya ngono.
“Nimepokea jumbe zaidi 5,763 na majina ya mashoga zaidi ya 100 hii inaonyesha WanaDSM hawataki laana ya mashonga. Naendelea kupokea majina ya Mashoga,” amesema Makonda.
Makonda amesema msako mkali wa kamata kamata ya mashoga na watu wanaojiuza utaanza wiki ijayo kwani kwa sasa anakiandaa kikosi kazi pamoja na kupokea baadhi ya majina.
Leave a comment