Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Olengurumwa afikisha kilio kwa Rais Samia
Tangulizi

Olengurumwa afikisha kilio kwa Rais Samia

Spread the love

 

ONESMO Olengurumwa, Mratibu Mkazi wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, afute zuio la wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito, kurudi shuleni baada ya kujifungua.Anaripoti Mwandishi Wetu, Shinyanga…(endelea).

Olengurumwa ametoa ombi hilo leo Jumapili tarehe 23 Mei 2021, katika ziara yake ya kutembelea wadau wa THRDC, mkoani Shinyanga.

Mratibu huyo wa THRDC, ameshauri Serikali ya Rais Samia, irekebishe sheria zinazowakwamisha watoto wa kike kuendelea na masomo, hasa wanaopata ujauzito wakiwa shuleni.

“Tumekuwa tukilalamika kuna sheria zinasababisha changamoto, hizi sheria ziwekwe vizuri ziweze kusaidia watoto wa kike. Mfano binti kurudi shule ni jambo la msingi sana anapopata ujauzito, nadhani Rais Samia tumuombe ahakikishe kwamba binti anapopata changamoto hiyo anarudi shule,” amesema Olengurumwa.

Zuio la wanafunzi wanaopata ujauzito kurudi shuleni baada ya kujifungua, liliwekwa 2017 na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dk. John Magufuli, ambaye aliagiza wanafunzi hao wajiunge na Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA).

1 Comment

  • Ni Jambo jema tena la kufikiriwa Sana, kama ilivyo kanuni na taratibu za ajira nchini KWA Sheria iliyopo ya kumzuia mtoto WA kike kuendelea na masomo baada ya kupata mimba, Sheria hii inawanyima watoto WA kike kupata ajira serikalini na maeneo mengine, pia inakiuka Haki na matakwa ya Kimataifa ya kukomesha Ukatili Dhidi ya Wanawake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!