Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Oil yaokoa maisha ya Mhandisi kivuko cha MV Nyerere
Habari MchanganyikoTangulizi

Oil yaokoa maisha ya Mhandisi kivuko cha MV Nyerere

Spread the love

OIL imetajwa kuwa miongoni mwa sababu zilizookoa maisha ya Mhandisi wa Kivuko cha MV Nyerere, Alphonce Charahani, aliyeokolewa akiwa hai baada ya kupita saa 48 tangu kivuko hicho kizame katika Ziwa Viktoria. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Wakizungumza baada ya kumuokoa mhandisi huyo, asubuhi ya leo tarehe 22 Septemba 2018, baadhi ya waokoaji walisema mbinu ya Mhandisi Charahani ya kujipaka oil mwilini, ilimsaidia kuzuia maji ya ziwa hilo kuingia kwenye vinyweleo vyake.

Kivuko hicho kilizama kwenye ajali iliyotokea tarehe 20 Septemba 2018 wakati kikisafirisha abiria kutoka kisiwa cha Bugorora kwenda Kisiwa cha Ukara kwenye Ziwa Victoria.

Baada ya kuokolewa, Mhandisi Charahani alikimbizwa katika Kituo cha Afya cha Busya kilichopo kisiwani Ukerewe kwa matibabu zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!