Chongolo alisema hayo wakati akizungumza na wanachama wa CCM shina namba tano wilayani Ulanga ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku tisa Mkoani Morogoro yenye lengo la kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo.
Chongolo alisema ni vema ofisi za mabalozi na Mashina zikatumika kwa kufanya vikao vya wazazi na watoto wao kubaini changamoto za watoto na vijana na kuona namna ya kuzipatia ufumbuzi.
Aidha alisema wazazi wananafasi kubwa ya kuwalea watoto katika misingi ya Mila na tamaduni walizokulia wao na hivyo kupata vijana bora wasioweza kujiingiza kwenye vitendo viovu ikiwemo kuwaibia wazazi wao.
Aidha aliitaka jamii kufuatilia na kuzingatia elimu inayotolewa bure na Serikali kupitia vyuo vya ufundi stadi VETA hapa nchini kwa vijana ikiwa ni lengo la kusaidia vijana kupata ajira binafsi na kutojiingiza kwenye makundi ya vishawishi vya wizi au udokozi.
“Rais Samia ametenga nafasi kwa ajili ya wanafunzi wanaomaliza masomo ya shule za msingi kuendelea na elimu ya ufundi katika vyuo vyote vya VETA nchini, hata kama wazazi wao hawana uwezo wa kuwapeleka vyuoni” Alisema Chongolo.
Awali katibu wa shina namba tano Raphael Boma alisema kumeibuka matukio mengi ya wizi au udokozi wa wanyama wafugwao nyumbani, vyakula na mashambani Mambo yanayofanywa na makundi ya vijana ndani ya wilaya hiyo.
Leave a comment