Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ofisi za mabalozi wa mashina zitumike kuwale vijana kimaadili – Chongolo
Habari za Siasa

Ofisi za mabalozi wa mashina zitumike kuwale vijana kimaadili – Chongolo

Spread the love
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo ameagiza ofisi zote za mabalozi wa mashina nchini zitumike kuwalea na kuwajenga watoto katika misingi ya maadili ya kitanzania kama njia rahisi ya kuimarisha usalama wao na mali zao. Anaripoti Christina Haule,Ulanga … (endelea).

Chongolo alisema hayo wakati akizungumza na wanachama wa CCM  shina namba tano wilayani Ulanga ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya siku tisa Mkoani Morogoro yenye lengo la kuimarisha chama na kukagua miradi ya maendeleo.

Chongolo alisema ni vema ofisi za mabalozi na Mashina zikatumika kwa kufanya vikao vya wazazi na watoto wao kubaini changamoto za watoto na vijana na kuona namna ya kuzipatia ufumbuzi.

Aidha alisema wazazi wananafasi kubwa ya kuwalea watoto katika misingi ya Mila na tamaduni walizokulia wao na hivyo kupata vijana bora wasioweza kujiingiza kwenye vitendo viovu ikiwemo kuwaibia wazazi wao.

Aidha aliitaka jamii kufuatilia na kuzingatia elimu inayotolewa bure na Serikali kupitia vyuo vya ufundi stadi VETA hapa nchini kwa vijana ikiwa ni lengo la kusaidia vijana kupata ajira binafsi na kutojiingiza kwenye makundi ya vishawishi vya wizi au udokozi.

“Rais Samia ametenga nafasi kwa ajili ya wanafunzi wanaomaliza masomo ya shule za msingi kuendelea na elimu ya ufundi katika vyuo vyote vya VETA nchini, hata kama wazazi wao hawana uwezo wa kuwapeleka vyuoni” Alisema Chongolo.

Awali katibu wa shina namba tano Raphael  Boma  alisema kumeibuka matukio mengi ya wizi au udokozi wa wanyama wafugwao nyumbani, vyakula na mashambani Mambo yanayofanywa na makundi ya vijana ndani ya wilaya hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!